NAMNA YAKUTUMIA TANGAWIZI KAMA TIBA

Kutibu kutokusagika kwa chakula tumboni, Gesi tumboni, Msokoto wa tumbo (bila kuharisha), Kutapika, Mshtuko/Mkazo wa ghafula (wa msuli),Maumivu ya tumbo na Kibofu cha mkojo ikiambatana na Homa, Mafua, Kukohoa na Pumu.TUMIA JAM YA TANGAWIZI.

JINSI YA KUTENGENEZA JAM YA TANGAWIZI:
Kamua TANGAWIZI mbichi kisha changanya maji yake (Juice) na Sukari. Chemsha mpaka mchanganyiko huo uwe mzito. Ongeza Zafarani iliyosagwa,Iliki iliyosagwa, Kungumanga zilizosagwa na karafuu iliosagwa. Iweke dawa hii vizuri na tumia inapo hitajika.

KWA KUVIMBIWA NA KUTAKA HAMU YA KULA.
Changanya Juice ya TANGAWIZI, Juice ya Limau na Chumvi Mawe kwa vipimo vilivyo sawa. Hakikisha umechanganya vizuri. Kunywa dawa hii kabla ya Chakula.Vingineyo changanya vipimo vilivyo sawa sawa vya Juice ya TANGAWIZI na Sukari Mawe. Koroga vizuri, kunywa kabla ya kula chakula. Dawa hii husafisha Ulimi na Koo na hukuongeza hamu ya kula na kukufanya mchangamfu.

MAUMIVU YA KOO NA KUKAUKA SAUTI.
Tafuna vipande vidogo vya Tangawizi.

KWA KUHARISHA.
Chua sehemu zinazozunguka kitovu kwa Juice ya Tangawizi.

KWA KISUKARI.
Kunywa Juice ya Tangawizi iliyochanganywa na Sukari mawe.

KIUNGULIA, KUKOSA HAMU YA KULA NA BAWASIRI.
Tumia Samasarkara Churna.

KICHEFUCHEFU NA KUTAPIKA.
Kunywa mchanganyiko wa Juiceya Tangawizi na Juice ya Kitunguu.

MAUMIVU YA KICHWA CHA WASIWASI.
Changanya Juice ya Tangawizi na Maziwa, kisha kausha. Nusa unga huo kama Tumbaku.

MAUMIVU MAKALI YA TUMBO.
Changanya kijiko kimoja cha au viwili vya Tangawizi iliyosagwa na kijiko kimoja au viwili vya mafuta ya Kastoroli. Kunywa kijiko kimoja mara mbili kwa siku.

BARIDI YA BISI SUGU.
Changanya kijiko kimoja cha Tangawizi ya unga na vijiko 24 vya maji kunywa mchanganyikohuu ukiwa vuguvugu. Ulale na ujifunike mpaka utoe jasho.

KUUMWA JINO NA MAUMIVU YA KICHWA.
Chukua Tangawizi ya Unga koroga na maji kidogo iwe nzito kama tope. Jipake na uchue kwenye paji lako la uso kabla ya kulala. Kwa Jino jipake na uchuwe kwenye Shavu.